#FAHAMUZAIDIMEDIA #DARUSOMLIMANI #UDSM
Rais wa serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha Dar es Salaam Mhe. Godwel Paulo, mnamo
tarehe 06 Juni, 2021 alilihutubia na kulizindua rasmi bunge la DARUSO MLIMANI kwa
mwaka wa masomo 2021/2022 mnamo saa 7:00 mchana katika ukumbi wa ATB.
Shughuli hii ilihudhuriwa na Ofisi ya mshauri wa wanafunzi mama Paulina Mabuga,
baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa DARUSO wanaomaliza muda wao wakiongozwa
na Mhe. Noel Mtafya pamoja na Waziri Mkuu mstaafu ndugu Abdulrahman Makere
sambamba na wafuatiliaji wa siasa za DARUSO na wanafunzi mbalimbali wa Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam.
Mhe. Rais alitumia fursa hii kutoa shukrani zake za dhati kwa umma wa wanafunzi wote
wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kumuamini na kumchagua kuwa Rais wa Serikali
ya Wanafunzi DARUSO MLIMANI na kutoa dira na muongozo wa serikali yake kuwa
itajikita zaidi katika kuwatumikia wanafunzi wote wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
pasipo ubaguzi wa aina yoyote ile katika viwango vya hali ya juu zaidi haswa kwa
kuzingatia vipaumbele vifauatavyo; umoja, amani na usalama, utawala bora,
ushirikishwaji wa wanafunzi wa uzamili na umahili, sanaa na michezo pamoja na
mahusiano baina ya taasisi za Chuo kikuu cha Dar es Salaam pamoja na zile zilizoko nje
ya chuo chetu.
Vile vile Mheshimiwa Rais aliwasilisha jina la Waziri Mkuu ambapo ndugu Ridhiwani
Maulid kutoka Ndaki ya Insia (COHU) ambaye pia awali alikuwa ni Mbunge mteule wa
Rais alipitishwa na bunge kwa asilimia mia moja (100%) kuwa Waziri Mkuu wa serikali
ya wanafunzi chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa mwaka wa masomo 2021/2022. Vile vile mheshimiwa Rais alisisitiza umoja na mshikamano miongoni mwa viongozi wote
waliopata nafasi ya uwakilishi wa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na
kuwahimiza kufanya kazi kwa weredi mkubwa na kuwaahidi wana DARUSO wote
wategemee mambo makubwa na utekelezaji mzuri kutoka katika serikali anayokwenda
kuiongoza.
Vile vile mheshimiwa Rais alitumia bunge tukufu la DARUSO kutangaza Baraza jipya la
Mawaziri likijumuisha jina la Katibu Mkuu Kiongozi, mawaziri katika wizara mbalimbali,
manaibu waziri, makatibu wa wizara pamoja na EX-COMS wa Rais kama ifuatavyo:
1. Mhe. Rais amemteua ndugu Joseph Mathias kuwa Katibu Mkuu kiongozi
serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COSS).
2. Mhe. Rais amemteua ndugu Christopher Titus kuwa Waziri, wizara ya
katiba, sheria na utawala bora (UDSOL) ambaye pia ni mbunge mteule wa
Rais.
3. Mhe. Rais amemteua ndugu Tillya Madeline kuwa Naibu waziri, wizara wa
katiba, sheria na utawala bora (UDSOL).
4. Mhe. Rais amemteua ndugu Simbila Dani kuwa Waziri, wizara ya Elimu
(COHU).
5. Mhe. Rais amemteua ndugu Alphonsina Ambrose kuwa Naibu waziri,
wizara ya elimu (IKS).
6. Mhe. Rais amemteua ndugu Nirabi Absalom kuwa Katibu wizara ya Elimu
(CONAS).
7. Mhe. Rais amemteua ndugu Miseyeki Kijana kuwa Waziri, wizara ya
Mikopo (COSS) ambaye pia ni mbunge mteule wa Rais.
8. Mhe. Rais amemteua ndugu Mwandu Geofrey kuwa Naibu waziri, wizara
ya mikopo (COAF).
9. Mhe. Rais amemteua ndugu Kereto Oinoti kuwa Katibu wizara ya mikopo
(COHU).
10.Mhe. Rais amemteua ndugu Otieno Evance kuwa Waziri, wizara ya Fedha
na uwekezaji (CONAS).
11.Mhe. Rais amemteua ndugu Ziwiyani Aman kuwa Naibu waziri, wizara ya
Fedha na uwekezaji (UDBS).
12.Mhe. Rais amemteua ndugu Kishasha Ashrafu kuwa Waziri, wizara ya Afya
na cafeteria (SOED) ambaye pia ni mbunge mteule wa Rais.
13.Mhe. Rais amemteua ndugu Umwelu Mohammed kuwa Naibu waziri,
wizara ya Afya na cafeteria (CONAS).
14.Mhe. Rais amemteua ndugu Aman Abraham kuwa katibu wizara ya afya na
cafeteria (UDSOEC).
15.Mhe. Rais amemteua ndugu Mohamed Mahmud kuwa Waziri, wizara ya
Ulinzi na usalama (IDS).
16.Mhe. Rais amemteua ndugu Mangula Philipo kuwa Naibu waziri, wizara ya
ulinzi na usalama (SOAF).
17.Mhe. Rais amemteua ndugu Munira Ally kuwa Waziri, wizara ya Habari,
jumuiya ya wanafunzi na mambo ya nje (COICT).
18.Mhe. Rais amemteua ndugu Tandika Robert kuwa Naibu waziri, wizara ya
habari, jumuiya ya wanafunzi na mambo ya nje (SJMC).
19.Mhe. Rais amemteua ndugu Lopa Christantus kuwa Waziri, wizara ya
michezo na burudani (SOED).
20.Mhe. Rais amemteua ndugu Mlay Brighton kuwa Naibu waziri, wizara ya
michezo na burudani (COET).
21.Mhe. Rais amemteua ndugu Chimwenda Wilson kuwa katibu wizara ya
michezo na burudani (COHU-Creative Arts).
22.Mhe. Rais amemteua ndugu Dorcas Gwilenza kuwa Waziri, wizara ya jinsia
na makundi maalum (COHU) ambaye awali alikuwa ni mbunge mteule wa
Rais.
23.Mhe. Rais amemteua ndugu Shinon Muhoja kuwa Naibu waziri, wizara ya
jinsia na makundi maalum (CONAS).
24.Mhe. Rais amemteua ndugu Rutayuga Prosper kuwa Waziri, wizara ya
usafirishaji na miundombinu (COET).
25.Mhe. Rais amemteua ndugu Mpumpa Jackson kuwa Naibu waziri, wizara ya
usafirishaji na miundombinu (SOMG).
26.Mhe. Rais amemteua ndugu Masiko Daniel kuwa Waziri, wizara ya maji,
malazi na mazingira (IKS).
27.Mhe. Rais amemteua ndugu Abdallah Husna kuwa Naibu waziri, wizara ya
maji, malazi na mazingira
(COSS).
28.Vile vile Mhe. Rais amemteua ndugu Masanja Alphayo kuwa Mwakilishi wa
wanafunzi wanaoishi nje ya chuo yaani OFF-CAMPUS.
Uteuzi huu ulianza rasmi jana tarehe 06 Juni, 2021 na tayari washaapishwa rasmi kwa
majukumu ya kuwatumikia wan


COMMENTS