Hii ni mara baada ya kutolewa kwenye mashindano ya EURO20 katika hatua ya kumi na sita bora dhidi ya swazirland na kushindwa kutinga hatua ...
Hii ni mara baada ya kutolewa kwenye mashindano ya EURO20 katika hatua ya kumi na sita bora dhidi ya swazirland na kushindwa kutinga hatua ya robo fainali
Wachezaji wa timu ya taifa ya ufaransa wameonekana wakiingia katika marumbano mara baada ya kuaga mashindano ya EURO2020 ikidaiwa kuwa mchezaji Kylian mbappe ambaye alikosa mkwaju wa penati katika mtanange dhidi ya swazirland na kuwakosesha nafasi ufaransa katika katika hatua ya robo fainali amedaiwa kuingia katika marumbano na mchezaji mwenza antoine Griezman huku sababu ikidaiwa kuwa ni wivu .kinachoelezwa ni kwamba antoine griezman ni maarufu sana katika taifa lake kuliko kylan mbappe hali ambayo inaibuwa mtafaruku baina ya wachezaji hao.kabla ya hapo siku za karibuni mbappe alidaiwa kuingia katika marumbano na oliver Giroud.sanjari na hilo pia imedaiwa kuwa kiungo wa timu hiyo paul pogba naye yupo katika marumbano na kiungo mwenzie Adrien Rabiot katika vyumba vya kubadilishia nguo katika baadhi ya mechi walizokuwa wakicheza, na sio kwa wachezaji tu lakini pia hata baadhi ya wazazi wa wachezaji timu hiyo wameonekana wakiingia katika marumbano wakati wanatazama Watoto wao wanachofanya uwanjani

COMMENTS